Kongamano la Miiraji Tarehe 25/05/2014 saa 2:00 asubuhi Ukumbi wa CCM Mkoa - Arusha. More... Click Here!


Tuesday, 29 July 2014

ARUSHA WAKISHEREKEA IDILFTR

BAADHI YA WAISLAAMU WAKITOKA KUSWALI SWALA YA IDI KTK MSIKITI WA SHAMSI-ARUSHA

MZEE SEHA NA RAFIKI ZAKE WAKIPATA KIFUNGUA KINYWA BAADA YA KUTOKA KWENYE SWALA YA IDI

Sunday, 27 July 2014

MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN YALIYO ANDALIWA NA MADRASAT SHAMSIL MAARIF MKOA WA ARUSHA


USATDH MASOUD AKIWA NA BAADHI YA WAUMINI

HAWA NDIO MAJAJI WA MASHINDANO HAYA

MSHINDI WA PILI WA JUZUU SITA AKICHUKUA ZAWADI YAKE

SHEIKH KHALIFA AKIFUATIWA NA USTADH KHALID NA DK.AKIL

PICHA YA PAMOJA YA WANAFUNZI WA SHAMSIL MAARIF BAADA YA MASHINDANO YA QUR-AN

BAADHI YA  WALIOHUDHURIA MASHINDANO HAYO


BAADHI YA WASHIRIKI WA MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN

Saturday, 26 July 2014

MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN YANAYO ENDELE HIVI SASA KATIKA WILAYA YA MONDULI

Ni ndani ya ukumbi wa C.D.T.I Wilayani hapa leo tarehe 26/7/2014 sawa na Ramadhan 28/1435 H.
MADRASAT SALAAMAT-ISLAAMIYYA ikiwa ndio waandalizi wa mashinadano hayo kama ambavyo tunamuona Sheikh Hussein mkuu wa madrasa  hiyo akiwakaribisha wageni wote katika mashindano hayo
SHEIKH HUSSEIN
ZAIDAN BINT RAMADHAN { MSHIRIKI WA JUZUU MOJA}
MSHIRIKI WA JUZUU MOJA
HUU NDIO UKUMBI ULIO TUMIKA KTK MASHINDANO HAYO

BAADHI YA WASHIRI WA  MASHINDANO HAYO NI KUTOKA MTOWAMBU,RAUDHWA KISONGO,SHAMSIL MAARIF ARUSHA  T.M.A NA WENYEJI WAO SALAMAT ISLAAMIYYA  HAPA MONDULI



Friday, 25 July 2014

MAADIMISHO SIKU Y A QUDS YALIYO FANYIKA KTK UKUMBI WA CCM MKOA ARUSHA

SHEIKH  ABULRAZAQ AKITOA NASAHA SIKU YA QUDS Habari kamili badae

BAADHI WA WAISLAMU SIKU YA QUDS

SHEIKH WA MKOA WA ARUSHA AKITILIA MKAZO MADA ZA WASEMAJI WALIO TANGULIA

Waislamu Arusha wakiadhimisha siku ya Qudsi mshuko wa swala ya ijumaa ktk ukumbi wa ccm Mkoa wenzetu Palestina waandamana


polisi wakabiliana na raia Palestina
Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel.
Waandamanaji hao wakiwa na hasira wakiwa Gaza walipambana na vikosi vya usalama vya Israel.
Hata hivyo mapambano makubwa dhidi ya vikosi vya usalama ilikuwa katika eneo la Qalandia katika mpaka wa Ramallah and Jerusalem.
Raia mmoja wa Palestinian ameuawa katika maandamano hayo huku wengine kadhaa wakijeruhiwa .
Takriban wapaelestina 800 wameuawa tangu kuanza kwa mashambulizi ya Israel huko Gaza mapema mwezi huu.

Sunday, 20 July 2014

MASHINDANO YA QUR-AN MKOA WA ARUSHA YANAYOENDELEA KTK UKUMBI WA CCM MKOA KUANZIA HIVI SASA MPAKA JIONI ENDELEA KUFUATILIA KUPITIA BLOG HII ILI UYAPATE KWA UKAMILIFU

IMARAN SAIDY MSHIRIKI WA JUZUU TATU

 MASHINDANO HAYA YALIANZA NAKUNDI LA JUZUU TATU  AMBALO KUNDI HILO LILIKUWA NA WASHIRIKI SITA AMBAO NI :-Bilal Salmin,Imran Saidy,Muhammad Shuaibu,Nuhu Athuman,Fadhil Mussa na Halima Issa uu
     Baada ya kukamilika kundi `A` lilifuata kundi 'B` ambalo ni kundi la juzuu tano
MWAJUMA ABDURAHMAN HUYU NI MSHIRIKI WA JUZUU TANO
Na kundi hili lina washiriki nane
Baada ya kumalizika kundi la juzuu tano sasa hivi linaendelea kundi la juzuu saba

ANAE TUFUNGULIA KUNDI HILI NI JAZILA OMARY

WALIO KAA VITI VYA MBELE NI WASHIRIKI WAKIUME NA MWANAFUNZI  ALIYESHIKA KICHWA NIMEJARIBU KUMUULIZA NI VP MBONA UNASHIKA KICHWA AKANIMBIA ANAFIKIRIA NAMNA MASHINDANO YALIVHO KUWA MAGUMU ANASEMA HUENDA ASING`AMUE KITU NIMEJARIBU KUMPA MOYO KWA KUMWABIA UTAFANYA VIZURI USIWE NA KHOFU

ANAE TOKA KUSOMA HIVI SASA NI JAZILA OMARY
 Na baada ya kumalizika juzuu saba sasa hivi  tunaendela na juzuu kumi na atakae tufungulia kundi hili ni Abuharith Issa

HUYU NI MSHIRIKI WA JUZUU SABA KWA JINA NI KULTHUMU ALLY

MAJAJI WAKIENDELEA NA KAZI YAO WALIOPEWA ,ALIYESHIKA KIPAZA SAUTI NI SHEIKH HADIYU HUSSEIN LUKARANGA AKIFUATIWA NA MUDIYR WA AL-AZHAR MKOA WA ARUSHA SHEIKH RAJABU ALHAD FULUFIL NA ALIYE SHIKA KALAMU NI KATIBU WA UWASUWA SHEIKH HUSSEIN HASSAN MYUYI

MASHINDANO HAYA NI ENDELEVU KILA MWAKA UNAOMBWA KAMA UNAUKEREKETWA WA DINI FIKA AMANA BANK KWA KUCHANGIA KUPITIA AKAUNTI HIYO HAPO JUU


BAADHI YA KINAMAMA WALIOKAA KWA UTULIVU WAKISIKILIZA MASHINDANO YANAYO ENDELEA HIVI SASA

HAWA NI WANAFUNZI WA MADRASA MBALIMBALI WAKIWA KTK MASHINDANO HAYO

MC USTDH HUSSEIN ALLY AKIMKABIDHI RATIBA YA MASHINDANO MTANGAZAJI WA ARUSHA ONE BW.MPINGA KINGU

Saturday, 19 July 2014

Israel yaendeleza unyama wake huko Gaza


 
Wakimbizi wa Gaza

Maafisa wa Umoja wa mataifa katika eneo la Gaza wanasema kuwa idadi ya raia wa Palestina walioachwa bila makao na ambao kwa sasa wanatafuta makao kufuatia mashambulizi ya nchi kavu yanayotekelezwa na Israel sasa imeongezeka maradufu kutoka elfu ishirini na mbili hadi elfu arobaini.
Raia wengi wameelekea Magharibi mwa Gaza ili kutoroka mashambulizi ya Israel.
Baada ya utulivu siku ya ijumaa kuna ripoti kwamba mizingi ya israel imefanya mashambulizi mengine usiku kucha.
Zaidi ya raia 60 wa Palestina wakiwemo watoto tisa wanadaiwa kuuawa tangu kuanzishwa kwa oparesheni ya nchi kavu na hivyobasi kuongeza idadi ya watu waliouawa kufikia 300.
Jeshi la Israel linasema kuwa mwanajeshi mmoja wa Israel aliuawa siku ya ijumaa kufuatia ufyatulianaji wa risasi wa wenyewe kwa wenyewe.

Copyright @ 2014 UWASUWA.

Designed by Japhary | Japhary Juma