Kongamano la Miiraji Tarehe 25/05/2014 saa 2:00 asubuhi Ukumbi wa CCM Mkoa - Arusha. More... Click Here!


Monday, 15 October 2018

SEMINA YA WALIMU WA MADRASA KATA YA NAMANGA WILAYA YA LONGIDO

USTADHI SHAHIRAN SALUMU NASSORO AKIWA AMEVAA JAKETI LENYE MISTARI MIKONONI,AKIFUATIWA NA MENEYEKITI WA KATA YA NAMANGA MZEE ABUU A.ZUBERI,ANAYE FUATA NI MWALIMU ABUBAKAR MAMBOLEO WA MADRASA YA ISTIQAAMAH MTAA WA FIDOFOSI JIJINI ARUSHA,ANAYE FUATA AMBAYE ANAYE PERUZI SIMU YAKE NI SHEIKH RAMADAHAN MPANGALA SHEIKH (W) NAMANGA ANAYE FUATA NI MWL.TWAHA MOHAMED MPERA MWENYEKITI USAJILI UWASUWA ,ANAYEFUATA NI AMIM MUHIDIN RASHID ALIYE VAA SHATI LA DRARFT MWALIMU WA AL-HIDAYA ANAYEFUATA NI MZEE ALLY KASSU MWENEYE NDEVU NEUPE ,ANAYEFUATA MWENYE SUALI YA JINZI NI MWENYEKITI HALMASHAURI BAKWATA KATA YA LONGIDO NAWAMWISHO KABISA NI MWALIMU NASSORO HASSAN NASSORO MWALIMU WA MADRASA YA AL-HIDAYA ILIYOPO NAMANGA   .

WAWEZESHAJI WALIJIKITA ZAIDI KATIKA KUELEZEA MSHIKAMANO WA WALIMU KATIKA MAENEO YAO,NAMNA YA UTOAJI WA TAALUMA BORA NA DONDOO ZA MADARASA MBALIMBALI AMBAPO MWENYEKITI IDARA YA DA`AWA USTADHI MIRAJI KHAMIS ISSA ALIELEZEA UMOJA,USTADH TWAHA MOHAMED ALIELEZEA TAALUMA , USTADHI ABUBAKARI MAMBOLEO ALIELEZEZEA USHIRIKI NA NAFASI YA WAZAZI KATIKA MADRASA NA USTADH MASOUD HUSSEIN ALIELEZEA DONDOO ZA MADRASA .

WANASEMINA WENGI WALIPONGEZA SANA UMOJA WA WALIMU KWA SEMINA HIYO NAWENGI WALIKUWA NA SHAUKU YA KUJIUNGA KATIKA UMOJA HUO, WALIDADISI KWA KINA TARATIBU ZA UMOJA HUO NA ZAIDI WALIVUTIWA SANA PALE WALIPO SOMEWA KATIBA YA UMOJA KATIKA SURA YA PILI UKURASA WA KWANZA INAYOELEZEA MALENGO NA MADHUMUNI YA UMOJA HUO.
SEMINA AMBAYO ILIANZA MAJIRA YA SAA 5:00 ASUBUHI NA KUMALIZIKA SAA 9:30 ALASIRI BAADA YA SEMINA HIYO LILI TOLEWA TANGAZO KUHUSU MUHADHARA MKUBWA AMBAO UNATARAJIWA HKUFANYIKA JUMAPILI IJAYO PANAPO MAJALIWA YA M.MUNGU KUANZIA SAA 8:00 MCHANANA KUMALIZIKA SAA 12:JIONI HAPO NAMANGA .

NA HATIMAE SHEIKH MPANGALA ALIWASHUKURU SANA UMOJA WA WALIMU NA KUAHIDI KUWA WILAYA YAKE IKO TAYARI KUTOA USHIRIKIANO WA HALI NA MALI KATIKA KUPELEKA MBELE GURUDUMU HILI LA UMOJA PIA ALIPATA FURSA YA KUTANGAZA TANGAZO LA MHESHIMIWA MUFTI WA TANZANIA LINALOWAHUSU WAFUNGISHAJI NDOA KUWA MUFTI ANAWATAKA WAJISAJILI ONLINE .



Tuesday, 24 July 2018

MWALIKO WA DUA MAALUMU KWA WALIMU WOTE WA MADRASA JIJINI ARUSHA 27/7/2017 SIKU YA IJUMAA BAADA YA SWALA YA ALASIRI

KWENYE JENGO HILI NDIO MAKAO MAKUU YA UWASUWA
WALIMU WOTE WA MADRASA MNAENDELEA KUKARIBISHWA, KAMA AMBAVYO MLIVYO ANZA KUTAPATA TAARIFA ZA AWWALI ZA MIAALIKO MBALI MBALI KUPITIA KWA WANACHAMA WETU
 MUDA WA DUA HIYO NI BAADA YA SWALA YA ALASIRI .
 ITAKUWA NI VIZURI ZAIDI TUKISWALI KWAPAMOJA HAPO SHAMSI. 
  KWASIOWEZA KUFIKA KWADHARURA AU UMBALI TUNAWAOMBA HUKO MLIKO  TUSHIRIKIANE KATIKA DUA NA VISOMO MBALIMBALI  LENGO KUU NI KUWAREHEMU WALIMU WENZETU WALIOTANGULIA MBELE YA HAKI.
NYOTE MNAKARIBISHWA

Thursday, 1 March 2018

KATIBU WA UWASUWA MAREHEMU USTADH HUSSEIN HASSAN ALIKUWA NI NANI NA ALIYAFANYA YAPI ?

PIGO KUBWA WAMELIPATA WALIMU WA DINI PAMOJA NA WAISLAMU WA JIJI LA ARUSHA KWA KUONDOKEWA NA KIPENZI CHAO USTADH HUSSEIN
إِنَّا لِلّهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعون

 Al-maruhumu Ustadhi Hussein Hassan Rashid Myuyi (1977-2018) marehemu Hussein Hassan alizaliwa mwaka 1977 hapa mkoani Arusha ,maremu Hussein yeye amezaliwa kutoka katika familiya ya Mzee Hassan Rashidi na bi:Shamiymu binti Maulidi hapo mtaa wa makaburi ya baniyani, marehemu Hussein ni kijana wa pili kuzaliwa katika familiya ya mzee Hassan akiwa ametanguliwa na dada yake mkubwa aitwae Leyla bint Hassan,watatu akiwa ni mdogo wake aitwae Twaha bin Hassan,wanne akiwa ni Iliyasa bin Hassan na akifuatiwa na kitinda mimba wao aitwae Zamzam bint Hassan hawa watano wote ni watu wa tumbo moja katika familia ya mzee Hassan lakini kabla ya wao kuzaliwa wanao wakubwa zao watatu ambao wamechangia mama ambao ni bwana Yunusi Ally Yusufu Ally na Fatuma binti Ally Mkungu .

Marehemu Ustadh Hussein alianza harakati za kusoma dini akiwa na umri wa miaka sita yaani 1986 kama alivyo lielezea hilo Sheikh na Mwalimu wake wa kwanza Ustdhi Juma Salimu Tura nakulithibitisha hili ndugu yake na marehemu aitwae Iliyasa
MWALIMU WAKWANZA  WA MAREHEMU USTADHI HUSSEIN HASSAN AKIWA NYUMBANI KWAKE HAPO MTAA WA SHAMSI JIRANI NA MAKAO MAKUU YA UWASUWA JIJINI ARUSHA
Sheikh Juma anasema nilimpokea Ustdhi Hussein akiwa na umri wa miaka sita wakati huo Madrasa yetu ikiwa mtaa wa makaburi ya baniyani kwa Mzee Kisiju mwaka 1983 ambapo kundi lake likiwa ni la pili likiwa limetanguliwa na kundi la kwanza la kina Issa Cheupe.mwalimu Husssein alianza kusoma shule ya msingi mwaka 1986 katika Shule ya msingi Ngarenaro na kumaliza mwaka 1993.
Marehemu Hussein alilelewa na wazazi wake katika maadili ya Dini pamoja nakuwa alikuwa anasoma shule wakati huo huo alipenda kusoma madrasa kitu ambacho kwa baadhi ya watoto hakipo pia baadhi ya wazazi hawana kwa kisingizio cha kwamba mtoto hawezi kusoma shule na madrasa kwa pamoja,baada tu ya kumaliza shule ya msingi alidumu katika madrasat Nuuri mpaka pale Sheikh Abdulkadir Sufi alipo asisi madrasa yake mtaa wa shamsi, madrasa ambayo ilikuwa ikisimamiwa na walimu wawili (Sheikh Shaban bin Jumaa ambaye kwasasa ni Sheikh wa Mkoa wa Arusha  na mwenzake Sheikh Simba M.Khalfan) ndipo marehemu Hussein alihamia kwa muda na kwenda kusoma Madrsa hiyo ya shamsi na badae alirudi kuja kuendelea kusoma hapa madrsat nuuri wakati huo mwalimu Hussein nikijana "ndipo nilipo waita baadhi ya wazazi yaani Marehemu Mzee Hassan baba yake na marehemu Ustadh Hussein amabaye aliishafariki toka mwaka 2001,Mzee Juma Ndao,Mzee Hussein Mori na Mzee Hussein Mfipa .
Baada ya wazee hao kufika nikawapa fikra yangu kuwa hawa watoto wetu tuwatoe waende wakaongeze elimu tuwapeleke kusoma nje ya Arusha wakati huo Sheikh Abdallah Swalehe Suna akifundisha Madrasa ya Riyadhwa hapo kona ya Nairobi na Sheikh Sharifu akifundisha madrasa yake hapo msikitini ngarenaro katika msikiti mdogo waliafiki fikra yangu ndipo nikawaambia subirini kwanza nimfikishie Sheikh Siraji,baada ya kumfikishia Sheikh Siraji bin Salimu Nymbwa alikubali fikra hiyo na kuwaita wazee hao baada ya kuongea nao nakufikia muwafaka ndipo Sheikh Siraji M.Mungu amrehemu alianza michakato ya safari na baada ya kukamilika aliwapeleka Mambrui huko lamu Nchini Kenya kwa Sheikh Sharif Sayyid Muhammad Albedhi." wakaanza kusoma huko na badae walihamia Madrsat Najah kwa Sheikh Sharif Mwinyibaba huko waliendelea na masomo yao mpaka walipo maliza wakarudi kwa Sayyid Muhammad Albedhi kwa ajili ya kutaka baraka zaidi za Sheikh yaani walipo anzia kusoma baada ya kutoka Tanzania lakini wakati huo mwanafunzi mwenzao Saidi Hussein alikuwa ameisha katisha masomo yake waliobaki  ni Mzamilu Juma Ndao,Hajji Hussein Mfipa,Twaha(Salimu)Salimu Juma Tura na marehemu Ustadh Hussein Hassan.
Baada ya kukamilisha masomo yao waliruhusiwa kila mmoja arudi aliko toka ili akaendeleze kazi ya Dini.marehemu Ustadhi Hussein kabla ya kurudi rasmi aliamua kuongeza miaka mitatu (3) na baada kuikamilisha alirudi nyumbani kwa ajili ya kufanya kazi ya M.Mungu,
Tulimpokea kwa furaha na kuwa nae hapa Madrasat Nuuri baada ya muda kupita Mwalimu Hussein aliomba ruhusa kuwa amepata nafasi ya kusomehsa Nairobi nchini Kenya baada ya kunipa taarifa hiyo nilimkatalia asiende naye pasi na kinyongo alitii tukaendelea kuwa pamoja nae .
Baada ya Madrasa ya Sheikh Sharifu kusimama ndipo sisi tulihamia rasmi hapo msikitini na wakati huo aliisha kuja Ustadh Juma Yahya wote tukawa tunfundisha Madrasat Nuuri na madrsa ikazidi kunawiri.
Iipo fika mwaka 2001 Mzee Hassan Rashid Myuyi baba ya marehemu ustadh hussein alifariki na kipindi hicho kilikuwa kizito sana kwa familia ya Mzee Hssan lakini Ustadhi Hussein alijitahidi kuwafariji ndugu zake khususwani wadogo zake ambao walikuwa bado masomoni (Twaha na Iliyasa) kwani wao wakati huo walikuwa wanaendelea na masomo ya sekondari.
Marehemu Ustadhi Hussein ile desturi yake ya kupenda kusoma alikuwa bado anayo kwani ndoto yake ilikuwa katika elimu ya sekula pia japo afike chuo kikuu kwa hivyo baada ya kuwa amepata elimu ya dini kwa mara ya kwanza aliamua kujiunga na kozi ya Uwalimu katika Chuo cha Kirinjiko na baada ya kukamilisha kozi hiyo aliamua kuendelea kuifanyia kazi elimu aliyo ipata kwakuanza kufundisha dini katika Markazi ya Wamisri  ya Al-azhar Sharif ya Jijini Arusha wakati huo Mudiyr alikuwa ni Fadhwiylatu Sheikh Ally Mukhtaar M.Mungu amrehem
Mwalimu Hussein pamoja nakusomesha Madrsat Nuuri na Madrsat Azh-har bado alikuwa ni mwenye kupupia mambo ya kheri kwani wakati huo pia alikuwa ameisha jiunga na umoja wa walimu wa madrasa pia alikuwa kaimu katibu akiwa amekaimu nafasi ya katibu wa kwanza wa UWASUWA Ustadhi Haruna Abdalla na badae alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu kutokana na utendaji wake mzuri kwa hakika alikuwa mchapa kazi hodari.
Pamoja nakuwa na majukumu mengi hakukata tamaa katika kujiendeleza alimua kujiunga na program za qualifying test(qt)ambapo alisoma na kufaulu vizuri katika mitihani ya kidato cha nne na ulipo fika mwaka 2006 aliamua kuanza maisha mapya ya kuishi na mke kwa kufunga ndoa ambayo iliyefungisha ndoa hiyo alikuwa ni Al-Alaama Sheikh Ally Mukhtaar .
Wiki mbili kabla ya kufariki marehemu Ustadh Hussein alituhimiza wanauwasuwa kuwahamasisha walimu mbalimbali kuendelea kujiunga na umoja nakusisitiza kuwa umoja ni nguvu kama inavyoonekana chati aliyo iandaa ili twende nayo katika ziyara Wilayani Karatu.
 Siku sita kabla ya kufariki marehemu Hussein (katibu wa uwasuwa) aliitisha kikao cha dharura (19/2/2018) na Agenda ilikuwa ujennzi wa Msikiti wa kudumu wa Daarul Mustwafa kwa ufadhili kama ambavyo maandishi ya hati yake yanavyo onekana katika kikao ambacho kilikuwa nawajumbe kumi na mbili


  (Ustadh Omary Saidi,Hussein Hassan,Masoud Hussein,Athuman Hussein,Jabir Muhammad,Issa M.Kapama,Hussein Suleymaan Auf,Khalid Mustafa,Abubakar Mamboleo,Miraj Khamis katibu wa madrasa ya Darul Mustwafa na Mwalimu Yahya wa Madrsat Daarul Mustwafa).
HIKI NDICHO KILIKUWA KIKAO CHA MWISHO NA KATIBU WETU USTDHI HUSSEIN HASSAN MYUYI NA ILIKUWA NI ZAMU YA USTADHI ISSA KAPAMA KUCHANGIA MADA

Jambo laajabu lililo dhihiri siku hiyo wengi wa Walimu walijitahidi kupiga picha kitu ambacho si chakawaida kwenye vikao ambavyo huwa vinafanyika mara kwa mara, kumbe picha hizo zilikuwa ndio picha za mwisho tukiwa na katibu wetu Ustadh Hussein kama picha zinavyo onekana hapo chini.
WAKWANZA ALIYE VAA MIWANI NDIYE MAREMU KATIBU WA UWASUWA AKIFUATIWA NA MWENYEKITI WETU SHEIKH UMAR SAIDI AKIFUATIWA NA USTADHI ATHUMAN ALIYESHIKA TAMA NI USTADH JABIR NA TOKA MWANZO WA KIKAO HAKUONYESHA USHANGAFU MPAKA MWISHO WA KIKAO AKIFUATIWA NA USTADHI KHALID MUSTAFA




Siku moja kabala ya kufariki  
Namnukuu Ustadh Khalid Mustafa "Jana jioni mimi ,Mwenekiti na katibu wa UWASUWA tulikuwa kwa mwanasheria kwa ajili ya kukamilisha mkataba wa kumkabidhi muhisani kazi ya ujenzi wa msikiti kama kikao kilivyo tuagiza ili jumatatu tumkabidhi na kazi ianze ."
Marehemu Ustadhi Hussein amefariki siku ambayo idara ya da`awa (kufikisha ujumbe k.v mawaidha au nasaha n.k )kupitia katibu wake Ustadhi Miraji alikuwa ameisha tutangazia kuwa baada ya swala ya magharibi tutakuwa na ziyara ya Da`awa  Masjidi Nabawiy Mtaa wa Uswahilini ungalimited kwa Sheikh Ayoub na ataye wasilisha mada atakuwa ni Ustadh Issa Muhammad Kapama kutoka fidifosi,
kama ilivyo kawaida ya umoja huu kila siku ya jumapili baada ya swala ya maghrib huwa awakatembelea Misikiti mbalimbali ya Jiji la Arusha  marehemu  Ustadh Hussein pia alikuwa ameisha tia nia ya kwenda kwenye ziyara hiyo lakini saa chache kabla ya kuingia maghrib alitutoka baada tu ya mwenyekiti wa umoja Sheikh Umar Saidi Jour kuthibitsha kifo chake alijitahidi kumpata
katibu wa Idarara ya Da`awa ili asitishe ziyara na awafahamishe wanauwasuwa kuhusiana na msiba mzito ambao wameupata wana uwasuwa baada ya Idara kupata taarifa za msiba Idara ya Da`awa ililazimika kusitisha ziyara hiyo.
Aama kuhusu kifo chake nikama alivyo simulia kifo hicho Ustadhi Athuman Hussein ambaye pia ni mwanauwasuwa namnukuu "leo saa 4 asubuhi tulialikwa hapo sheli ya panoni kwa Mama Abdilahi kulikuwa na shughuli ya hakiki sote kwa pamoja tukiwa na marehemu Ustadhi Hussein kwa ajili ya hiyo sunna ya hakiki shughuli ambayo imemalizika saa 6 ya mchana baada ya hapo tulirudi haraka kwani tulikuwa na kikao kifupi cha harusi ya kijana wetu wa madrasa (Issa Ramadhan) ambaye anatarajia kufunga ndoa yake mwisho wa mwezi wa tatu 31/3/2018 baada ya hapo tulikwenda kwenye harusi ya Shafii Hamad Abdallah na bi Aziza Iddi hapa ngarenaro maeneo ya kibanda umiza baada ya muda kidogo Sheikh Mahamud Salimu Nyambwa aliingia na kumuagiza Ustadh Hussein aijaze kabisa hiyo hati ya ndoa Ustadhi Hussein alianza kujaza coppy ya kwanza na aliikamlisha alipoanza coppy ya pili alisema najisikia vibaya mara tu tukaona anaishiwa nguvu tukaanza kumpepea gari ikasogea tukampeleka Hospitali kwa babu Madakatari walimpokea na kuanza kumuhudumia mwisho wa yote walisema kuwa presha ilikuwa imepanda sana na baada ya dakika chache akawa amefariki inna lilahi waina ilaihi rajiun " 
marehemu alikufa siku ya jumapili jioni na kuzikwa siku ya jumatatu katika makaburi ya fidifosi.

Monday, 26 February 2018

MAZISHI YA KATIBU WA UMOJA WA WALIMU WA MADRASA MKOANI ARUSHA LEO JUMATATU 26/2/2018 SAWA NA TAREHE 10/JUMADA THAANI/1439 HIJIRIYYAH

MAMIA YA WAUMINI  NA WAKAZI WA JIJI LA ARUSHA KUMSINDIKIZA KATIBU WA  UWASUWA USTDHI HUSSEIN HASSAN MYUYI KATIKA NYUMBA YAKE YA MWISHO KATIKA MGONGO WA ARDHI ........... HABARI  KAMILI BADAE KIDOGO



Saturday, 10 February 2018

ZIYARA YA UMOJA WA WALIMU WILAYANI KARATU 10/2/2018

KIBAO KIKIELEKEZA MSIKITI WA KIBAONI ULIPO, AMBAPO MSIKITI HUO NDIO KILIKUWA KITUO CHA KWANZA KATIKA ZIYARA HIYO AMBAPO TULIKUTANA NA WENYEJI WETU KATIKA ZIYARA HIYO WAKIWA NA KIONGOZI WAO MKUU KAIMU SHEIKH WA WILAYA YA KARATU SHEIKH RAJABU BIN ALLY
SEHEMU YA MBELE YA MSIKITI WA KIBAONI MSIKITI AMBAO IMAMU WAKE NI KAIMU SHEIKH WA WILAYA
HII NI SEHEMU YA  UPANDE WA KULIA MWA MSIKITI HUO

BAADHI YA WAUMINI WA MSIKITI WA KIBAONI

USTADHI ABDUL SHABAN ANTA  AKIWASILISHA MADA YAKE ILIYOKUWA INAELEZEA KUHUSIANA KURIDHI QADARI NA HUKUMU YA ALLAH ( S.W )


BAADA YA SWALA SHEIKH RAJABU ALLY AKIAGANA NA USTADHI ABDUL

SHEIKH RAJABU AKIAGANA NA USTADH MASOUD


SEHEMU YA NYUMA YA MSIKITI  NA KATIKA ZIYARA HIYO BAADHI YA WALIMU WALIFIKA KARATU MJINI KWA SHEIKH ABUBAKAR,KILMATEMBO KWA SHEIKH SHARIFU 


Saturday, 24 June 2017

HIVI NDIYO YALIVYO KUWA MASHINDANO YA KUHIFADHI QUR-AN 29/RAMADHA/1438 SAWA NA 24/6/2017

Katika Mashindano hayo yaliyo shirikisha Madrasa nane ( 8 ) za Jijini Arusha mbazo ni Hidaya kutoka Olmatejo,Darul Qur-an kutoka Sombetini, Nuri kutoka Ngarenaro ,Manazilul Abraar kutoka kwa morombo, Arusha Islamic Center kutoka Majengo ,Abdurahmaan Bin Auf kutoka Olmatejo , Swafa kutoka Kaloleleni na wenywji wao  Shamsili Maarif kutoka Shamsi.
KIJANA ABDULHAKIMU MUHAMMAD ALIYE VAA KOFIA NYEUPE NDIYE ALIYE SHIKA NAFASI YA KWANZA KWENYE KUNDI HILI LA JUZUU MOJA NAKUZADIWA SH 50,000/=  ,ANAYE FUATA KATIKATI MTOTO AMANI AYOUB SHIJA ALIIBUKA KUWA MSHINDI WA PILI  NA ALIZADIWA SH 30,000/=NA KIJANA ABDULRAHIMU JUMA (ALOLOO) ALIBUKA KUWA MSHINDI WA TATU NA ALIZAWADIWA SH 20,000/=
Baadhi ya walio hudhuria katika mshindano hayo kama tunavyo waona na miongoni mwao ndio mara ya kwanza kushiriki mashindano ya qur-an hapo anaonekana mwanafunzi Amani Ayoub shija ( mshindi wa pili wa juzuu moja) akiwa ameinamisha kichwa chini akifiria hivi anaweza kufanya vizuri pia ukimtazama mwanafunzi Abdurahimu Juma Aloloo ( mshindi wa tatu wa juzuu moja )  akiwa ameshika mashavu huku akitafakari mchuano namana ulivyo kuwa mkali
Mzee Ally Kassu baada ya kustaafu mashindano ya kuendesha magari ameibukia kwenye mashindano ya kuhifdhi Qur-an na hapo akichukuwa zawadi baada ya kufanya vizuri katika mashindano hayo
Majaji wa masindanano hayo wakijumuisha max baada ya makundi yote manne kusoma aliyeshika kalamu ni Ustadhi Hussein Hassan Myuyi ambae ni katibu wa Umoja wa Walimu Mkoa Arusha anaefuata  ni Ustdhi Gingi anajumuisha max ambaye  ni mmoja miongoni mwa walimu wa kituo maarufu cha kuhifadhisha Quran Jijini hapa kituo cha abdurahmaan bini auf cha hapo olmatejo na anayefuata ni sheikh Hadiyyu Hussein Lukarange ambe yeye ni Naibu Mudiyr wa Markazi ya Azhar Sharif ya Jijini Arusha
kijana mwenye kanzu na kofia nyeupe (Thabiti Salimini) kutoka Shamsil Maarif aliibuka kuwa mshindi wa kwanza wa juzuu tatu na alizawadiwa sh 80,000/= na anae fuata mwenye kilemba chekundu kijana Saadat Abdullahi kitoka Taasisi ya Hidaya Olmatejo alikuwa mshindi wa pili wa juzuu tatu na alizawadiwa sh 50,000/=  na Bw.Mahmudu Sufiyan muendesha bodaboda maarufu wa kijiwe cha Shamsi aliweza kuipokonya nafasi ya tatu na alizawadiwa sh 30,000/=  katika mashindano ambayo yalikuwa na mchuano mkali  katika kundi hilo lililo shirikisha washiriki ishirini na moja (21)

kijana mdogo katikati ( Luqman mohamed ) kutoka kituo cha Abdirahmaan bin Auf  olmatejo Alijinyakulia nafasi ya kwanza na kuzawadiwa sh 100,000/= ,anaye fuatia  Kijana Hambali Hambali Mohamed aliye vaa kofia  kutoka Arusha Islamic Center alichuwa nafasi ya pili na kuzawadiwa sh 80,000/=  na kijana Issa Mohamed kutoka Madrasat Nuri Ngarenaro aliye vaa kilemba kichwani  alishika nafasi ya tatu na kuzawadiwa sh 50,000/=

Mshindi wetu wa kwanza katika kundi hili la juzuu tisa ( 9 ) alikuwa   ni Hamza bin Ally kutoka kituo cha tahfidhul Quran cha Abdurahman bin Auf hapo olmatejo na alizawadiwa sh 150,000/= nafasi ya pili ilichukuliwan na  Binti mdogo aliye vaa hijabu nyeusi ( Hajra bint Rashidi ) kutoka Darul Qur-an sombetini  alizawadiwa sh 100,000/=na nafasi ya tatu ilchukuliwa na Swaumu bint Issa Khamis kutoka shamsil maarif  alye vaa jilbabu rangi ya maziwa na ufito wa rangi ya kijani  naye alizawadiwa sh 80,000/=
Ustadhi Masoud Hussein Salimu aliye shika  microphone ambaye ndiye mratibu mkuu wa mashindano hayo kabla ya ugawaji wa zawadi alielezea kiufupi namna ambayo mashindano yao yanavyozidi kukuwa makubwa mwaka hadi mwaka na kutoa mwito kwa wahisani mbalimbali waweze kujitokeza kudhamini mashindano hayo ,
Naye naibu Mwenyekiti wa Umoja wa walimu Mkoani Arusha Sheikh Juma Haji Mtandaya wapili kutoka upande wa kulia alitoa msisitizo wa kuwa na mchujo kabla ya kufanya mashindano ya Qur-an kwani wako baadhi ya wanafunzi wanaingia kwenye mashindano ili hali ni wabovu hawana vigezo naakatolea mfano wenzetu Dar-es-salaam wao wanafanya mchujo mpaka mara tano hivyo basi anawaomba wanaoandaa mashindano haya ( shamsil maarif  ) mwakani watakapo andaa tena mashindano  wawafanyie mchujo kabla ya kuingia katika mashindano .
             Khalifa Abubakar Saidi aliye shika kichwa akimuwakilisha Sheikh Salimu Mubarack (Sayyid Sujjada ) ndiye alikuwa mgawaji zawadi kwa niaba ya sheikh kwa washindi na washiriki wa mashindano hayo


Sunday, 11 December 2016

SHEREHE ZA MAULIDI MKOANI ARUSHA KIMKOA ZAFANYIKA ARUSHA MJINI

WANAFUNZI WA MADRSA KAMAA ILIVYO KAWAIDA YAO KUTOKANA NA NAMNA WALIVYO FUNDISHWA KUMPENDA MTUME MUHAMMAD ( S.A.W ) WAO HAKUJALI KUPIGWA NA JUA WAO KILCHO WALETA NI MUSIFU MTUME PAMOJA NA KUMUADHIMISHA

BAADHI YA WALIMU WA UWASUWA WAKISHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE KUHAKIKISHA KUWA WANAFUNZI WOTE  WANAO HUDHURIA WANAMFURAHIYA MTUME KATIAK HALI SAWA

KATIBU WA UWASUWA AKIWA MSTARI WA MBELE KATIKA ZOEZI LA KUDHIBITI JUA KUTOKANA NA UMATI WA WAISLAMU WA JIJI LA ARUSHA AMBAO KILA BAADA YA DAKIKA CHACHE WALIKUWA WANAONGEZEKA

USTADH ABDILAHI IMAMU WA MSIKITI WA BONDENI AKISOMA DUA YA WASILATU SHAFIY

MGENI RASMI SHEIKH ALLY CHIZENGA AKIWASILISHA MADA YAKE

SHEIKH ISTAMBULI ABDILAHI NAASR AKIWAKILISHA MASHIA WA NCHI YA JIRANI YA KENYA KATIKA MAULIDI HAYO AMBAYO YALIALIKA WATU WOTE

UMOJA WA WALIMU PAMOJA NA KUSIMAMIA BAADHI YA MAMBO WAO KAZI KUBWA WALIYO PEWA NA BARAZA LA BAKWATA ILIKUWA NI KUSIMIA UTARATIBU MZIMA WA KUHAKIKISHA KILA ALIYE HUDHURIA ALITABARUKU HIVYO BASI WALILAZIMIKA BAADHI YAO KUFIKA KWA WAPISHI ILI KUANZA KAZI YAO RASMI NA ALHAMDULILAHI WALISIMAMIA VIZURI

WANAFUNZI WA MADRASA WAKISUBIRI KUHAMISHIWA JUKWAA LA JUU BAADA YA JUA KUWA KALI

NAE SHEIKH ABDURAZAK WA MKOANI HAPA AKIWAKILISHA MASHIA WA ARUSHA KATIKA MAULIDI YA MKOA

BAADHI YA MASHEIKH WA JIJI LA ARUSHA WAKIWA SAFU YA MBELE KAMA TUNAVYO WAONA UPANDE WA KULIA ALIYESIMAMISHA BAKORA YAKE CHINI NI SHEIKH SIMBA KHALFAN AKIFUATIWA NA SHEIKH KISUA ALLY AKIFUATIWA NA MGENI RASMI SHEIKH ALLY CHIZENGA KUTOKA DAR-ES-SALAAM AKIFUATIWA NA SHEIKH WA MKOA WA ARUSHA SHEIKH SHABAN JUMA AKIFUATIWA NA SHEIKH WA WILAYA SHEIKH ABDIRAHMAN SALIM

MWENYEKITI WA UWASUWA USTADHI OMARI SAIDI JOUR AKITAFSIRI BAADHI YA AYA ZA QUR-AN TUKUFU ILIYOSOMWA NA KIJANA OMAR IDDI ABEID

MC.SHEIKH HADIYU HUSSEIN LUKARANGE AKIPITIA RATIBA YAKE ILI KUHAKIKISHA MAMBO YANAKWENDA VIZURI

Copyright @ 2014 UWASUWA.

Designed by Japhary | Japhary Juma